Waziri wa habari ,Utamaduni, sanaa na Michezo nchini Tanzania amewapiga Stop washabiki wa Yanga ambao wamejipanga kwenda kuwazomea Simba watakapokuwa wakicheza leo dhidi ya JS Saoura
Mwakyembe alifunguka kuwa suala hili ni la kitaifa hivyo waliopanga kwenda kuizomea Simba basi wasifike uwanjani maana wanahitaji uzalendo kwanza.
“Wale mashabiki wanaotaka kwenda kuizomea Simba nawasihi wasifike uwanjani. Hili ni suala la kitaifa, uzalendo kwanza”
Licha ya waziri kutotamka Yanga lakini inaeleweka na imekuwa utamaduni kwa washabiki wa Yanga kwenda kuizomea Simba inapocheza na timu nyingine au Simba kuizomea Yanga inapocheza na timu nyingine.
No comments:
Post a Comment