Pamoja na mambo kumuendea vibaya akiwa na Man United, mambo yamezidi kumkaba kiungo Anderson.
Anderson ameamua kurejea Brazil na kujiunga na timu ya Internacional lakini juzi alijikuta akitolewa katika dakika ya 36 kutokana na kushindwa kupumua.
Kiungo huyo alitolewa kutokana na kuwa na matatizo ya kupumua kutokana na hali ya hewa ya eneo hilo wakati wakiivaa timu ya nchini Bolivia.
Bolivia imekuwa ikiwasumbua wanasoka wengi katika suala la pumzi kwa kuwa iko juu sana kutoka usawa wa bahari.
Baada ya kutolewa nje katika mechi hiyo ya Copa Libertadores, Anderson aliwekewa mashine ya kumsaidia kupumua.
No comments:
Post a Comment