BONDIA Manny Pacquiao amefanikiwa kumpata bondia wa kufanya naye mazozi ya kupimana uvabu, 'sparring partner' kutoka gym ya mpinzani wake, Floyd Mayweather kuelekea pambano lao lenye thamani ya Pauni Milioni 300 Mei 2, mwaka huu, kwa mujibu wa kocha wake, Freddie Roach.
Sasa anaamini amepiga bao zuri baada ya kumpata bondia wa kupimana naye ubavu, kutoka kambi ya mpinzani wake, Las Vegas gym ambaye amekataa kutajwa jina.
"Nina sparring partner wa siri," Roach amesmea. "Hataki kujulikana kwa kuhofia kuwekewa bifu kwa sababu ametoka kambi ya Mayweather,".
Pacquiao na Mayweather watakutana uso kwa uso Jumatano kwa ajili ya kulitangaza rasmi pambano lao kwenye Mkutano na Waandishi wa Habari.
Freddie Roach amesema amepata sparring partner kutoka kambi ya Floyd Mayweather
Manny Pacquiao anapiga ngumi begi lenye uzito mkubwa kuelekea pambano na Mayweather
No comments:
Post a Comment